Kampuni ya ving’amuzi ya StartTimes Kenya imeanzisha channel mpya inaitwa
Triple P ambayo itakuwa inahusika na kurusha material ya entertainment tu kutoka
Kenya kwa masaa 24. Triple P itapewa leseni rasmi na Music Copyright Society
of Kenya (MCSK) kucheza kazi za wasanii wa Kenya kwenye channel ya Triple P
ambapo
leseni hiyo watailipia kila mwaka. Kutokana na kulipia leseni hiyo,
kampuni ya
StarTimes pia inakuwa na nafasi ya kutoa na ruhusa au kibali cha wamiliki wa
maeneo kama supermarket,banks,malls,restaurant na sehemu kama hizo za wazi
kuonyesha channel hii kwa malipo maalum. Sehemu hizi channel hii itakuwa inaoneka
kwa jamii nzima bure, ambapo watu wengine watakuwa hawajalipia hiyo channel lakini wanaangalia. Malipo haya maalum kwa wamiliki wa eneo husika yanatokana na sababu
kama hii.
Mapato haya yote yataweza kuwafikia wasanii kutokana na leseni inayolipiwa kila
mwaka na kampuni ya Startimes kwenda Music Copyright Society of Kenya (MCSK).
Triple P itapatikana kwenye package zote za StarTimes
No comments:
Post a Comment