aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Friday, August 9, 2013

IDDI AZAN (Mbunge wa Kinondoni) ajibu uvumi uliosambaa kuwa anajihusisha na MADAWA YA KULEVYA

Yafuatayo ni maneno maswali na majibu aliyoyatoa kwenye interview na Mussa Hussein wa Jahazi Clouds FM.
d Azan ambae ni mbunge wa jimbo la Kinondoni ameongea kuhusu tuhuma nzito zilizosambaa kwenye mitandao baada ya kutajwa kwenye barua ya Mtanzania anaedai kufungwa gerezani Hongkong kwamba ni mmoja wa matajiri kwenye biashara ya dawa za kulevya Tanzania.
Vipi kuhusu hizi tuhuma Mheshimiwa?
“Hata mimi mwenyewe sijui tuhuma hizi wapi zimeanzia, ila nakumbuka mwaka  jana kuna baadhi ya viongozi wa CCM walisema kwenye mkutano wa vijana kwamba mimi najihusisha na biashara hii haramu. Nikachukua hatua ya kuwaatarifu polisi na waliwahoji wale watu kilichoendelea wanajua wao polisi kwasababu mimi niliwaachia wao. Lakini hivi sasa hili swala limejitokeza tena kwa namna nyingine. Kuna mfungwa ambaye sijui yupo China au Hongkong ameandika barua na ipo kwenye mtandao na watu wameshaanza kunihukumu. Kitu cha kwanza naweza kusema kwamba hii barua ni ya uongo, mimi sijihusishi na biashara ya madawa ya kulevya na wala sijawahi kujihusisha na biashara yoyote haramu. Kingine mfungwa mwenyewe hakusema yeye ni mfungwa namba ngapi au kafungwa gereza gani ili tuweze kumfuatilia atoe ushahidi zaidi. Hiki kitu mimi nimekichukulia hatua za kisheria, nimeitaarifu polisi juu ya hili swala tena. Hii ni mara ya pili nataka haki itendeke, mimi siko juu ya sheria natakiwa nifate sheria kama nahusika na hiyo biashara hatua zichukuliwe.”
Lakini kwanini ni wewe tu mara ya pili hii na sio waheshimiwa wengine?
“Hata sijui kwa nini mimi tu,chanzo nadhani kilianza kwanini anatembelea magari mazuri . Wakaanza kuuliza anafanya biashara gani huyu au anaunza unga au hivi na vile ndiyo ikawa hivyo.Labda jinsi ninavyojihusisha na wananchi wangu kwa karibu najichanganya pamoja nao labda hilo linawafanya waweze kuongea hivyo. Kingine jinsi ninavyokubalika kwenye jimbo langu, ukifuatilia kwa makini tuhuma iliyopita ilitoka wakati tunaelekea kwenye uchaguzi na hivi sasa tupo kwenye safari ya kuelekea kwenye uchanguzi tayari maneno kama haya yashaanza kutoka. Sasa kuna watu wananiogopa kwenye jukwaa kwamba nikisimama nao hawaniwezi kabisa sasa wanajaribu kunichafua ili kuniondoa kwa kuwambia wananchi kuwa mimi sifai. Huu ni ugomvi wa kisiasa sana.”
Mheshimiwa kama huu ugomvi ni wa kisiasa unadhani utakuwa unatoka ndani ya chama cha CCM au nje?
“Mimi naamini ni ndani ya CCM kwasababu waliotamka maneno haya hapo zamani ni viongozi wa CCM wakubwa tu tena ngazi ya mkoa pia hata kabla ya mwaka 201o kwenye uchaguzi wa kura za maoni kuna viongozi wa CCM pia walizungumza maneno haya.”
Vipi kuhusu wananchi wa Kinondoni ambao ndiyo wapiga kura wako ambao wamekutana na hali ya sintofahamu, nia bado ipo kwa mwaka 2015?

“Naomba niwaondoe wasiwasi wananchi wa Kinondoni, mimi nitaendelea kuwa mwadilifu kwenye kazi, siwezi kukiuka maadili ya kazi yangu. Kuhusu mimi mwaka 2015 ni mapema sana kuzungumzia. Lakini panapo majaaliwa ya kiafya basi tutagombea. Nikisema hivi najua watu hawa wanazidi kuumia kwasababu wanajua nikisisimama mimi jinsi nilivyokaribu na watu wangu lazima nitachukua kiti.”

No comments:

Post a Comment