Klabu ya Coastal Union imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa
kiganda Yayo Lutimba kutoka timu ya mamlaka ya mapato ya
Uganda URA.
Aliyefanikisha zoezi hilo ni meneja wa Wagosi, Akida Machai ambaye
amepanda ndege mpaka jijini Kampala kunasa saini ya kijana mdogo
mwenye miaka 19, Yayo Lutimba Kato kutoka timu ya mamlaka ya
mapato Uganda (URA).
Nassor Ahmed ‘Binslum’, ambaye ni mkurugenzi wa ufundi amesimamia
kwa kiasi kikubwa kufanikisha usajili wa wachezaji takriban tisa
ukijumlisha na Kato amezungumza na blog hii usiku wa leo baada ya
Meneja Machai kuenda kumtambulisha Kato kwa Binslum na kuweka
wazi kuwa tatizo la ukame wa mabao litaisha kwa wana Mangush.
Itakumbukwa kocha Mkuu wa Coastal Union, Hemed Morocco wiki chache
zilizopita wakati wa kujiandaa na mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya URA,
aliweka wazi bado kikosi chake kina matatizo ya umaliziaji.
Alibainisha kikosi hicho kipo vizuri kila idara kuanzia golikipa, mabeki na
viungo ila hakuna mtu mwenye uchu wa mabao hivyo kuahidi kuwatumia
wachezaji haohao kuwafundisha namna ya kuadhiri magolikipa wa
timu pinzani.
Ndiyo maana winga Danny Lyanga alikuwa akichezeshwa namba kumi ili
kumuangalia uwezo wake wa kupachika mabao lakini hakuonekana kucheza
vema kwenye mechi ya URA.
Kwa usajili wa miaka miwili kuitumikia Coastal Union kinda huyu atakuwa
na nafasi nzuri sana kujitengenezea jina nchini Tanzania hasa baaada ya
kuwa na rekodi nzuri ya kuwafunga Simba na Yanga mabao mawili
mawili katika mechi walizokutana nazo kwa vipindi tofauti.
Zipo taarifa kuwa Yanga nao walikuwa mbioni kumnyakua kinda
huyu lakini Meneja Akida Machai amewazidi akili kwa kumfuata
hukohuko kwao Uganda. Na hizi ni mbinu za ‘kimafia’ zinazotumiwa
na timu kubwa duniani kote kunasa wachezaji mahiri.
Mungu akipenda kesho Kato ataungana na wachezaji wenzake
katika kambi iliyopo pembezoni mwa bahari ya hindi Raskazone
Hotel, jijini Tanga.
Wagosi wameanza vizuri mechi zao mbili za majaribio ambapo
mechi ya kwanza walishinda bao 1-0 dhidi ya URA na siku tatu
baadaye wakashuka dimbani dhidi ya Simba SC ambao nao
walichapwa 1-0. Zipo taarifa za kucheza mechi ya kirafiki
siku ya Eid pili uwanja wa Mkwakwani lakini zikishathibitishwa
na timu tutakayocheza nayo tutawahabarisha.
No comments:
Post a Comment