WATU wanne wa familia moja wamefariki na wengine 13
wamelazwa hospitalini kutokana na kula chakula chenye sumu
wakati wa sikukuu ya Idi el Fitri.Watu hao wamelazwa
wakati wa sikukuu ya Idi el Fitri.Watu hao wamelazwa
Kituo cha Afya cha Lusewa wilayani Namtumbo na Hospitali ya
Serikali ya Mkoa wa Ruvuma (HOMSO).
Kamanda wa Polisi Mkoa Deusidebit Nsimeki, alisema tukio hilo
lilitokea Agosti 9, mwaka huu saa 7:00. Kamanda Nsimeki,
alisema siku hiyo kabla ya tukio, Salum Mumba, alinunua samaki
aliyepeleka nyumbani kwa ajili ya sikukuu ya Idi.Kamanda
Nsimeki alisema katika tukio hilo Polisi wanamshikilia
mtu mmoja ambaye hakutaka kumtaja jina ambaye atasaidia polisi
kwenye upelelezi wake.
Alisema baada ya kula chakula hicho, haikuchukua muda mrefu
mtoto alianza kuumwa naye baadaye alifariki dunia. Baadaye
watoto wawili walianza kuumwa na kufariki. Watu wengine 13
walianza kuumwa baadaye majirani walipata taarifa kuwakimbiza
watu hao hospitali.
Aliwataja waliolazwa katika kituo cha afya cha Lusewa kuwa ni
Tazamio Mumba, Zidani Mumba, Ramadhani Mumba na Zahara
Mumba wote wakazi wa kitongoji Tulieni B.
Waliolazwa katika hospitali ya Mkoa wa Songea kuwa ni Gairi
Mumba, Zamoni Mumba, Fatuma Rashidi, Samidu Mumba, Asha
Omary na Sharifa Mumba.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi ya Hospitali ya Mkoa Songea Dkt. Benedictor Ngaiza alisema wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo hali zao zinaendelea vizuri.
No comments:
Post a Comment