aaaaa

Pages

Ads 468x60px

Monday, August 12, 2013

BOT YAONYA MATUMIZI YA NOTI BANDIA...



BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) Kanda ya Kaskazini, Arusha imewatahadharisha wananchi kuhusiana na tatizo la noti bandia nchini, anaripoti Richard Konga, Arusha.Akizungumza wakati wa Maonesho ya Wakulima Nane nane yaliyomalizika hivi karibuni, Meneja wa Fedha na Utawala wa BoT, Evena Ndesingo, alisema benki hiyo imeanza kutumia maonyesho ya wakulima kutoa elimu ya utambuzi wa noti zake
Alisema wananchi wanatakiwa kuwa makini wakati wa kutoa au kupokea fedha ili kuepuka kufilisika na kuyumbisha uchumi wa taifa.“Benki imeanzisha utaratibu wa kutoa elimu kwa wananchi ili watambue noti bandia kupitia alama halisi zilizoko kwenye noti halali,” alisema.
Hata hivyo, alisema matumizi ya noti bandia ndani ya jamii yanapungua kila mwaka kutokana na jamii kuwa na uelewa wa noti halisi na bandia na hivyo kupunguza kasi ya mzunguko wa noti bandia hizo.
Alisema BoT kupitia matawi yake nchini imejidhatiti kuwaelimisha wananchi juu ya utambuzi wa noti mpya na alama zake ili jamii izielewe na kutofautisha noti hizo.Alisema noti bandia iwapo zitaachwa ziendelee kuwepo kwenye mzunguko wa matumizi ya kawaida ipo hatari kwa jamii kufilisika na taifa kuyumba kiuchumi.
Ndesingo aliwataka wananchi kuwa makini wanapofanya malipo ya noti mpya kwa kuchunguza kwa makini alama hizo kabla hazijapelekewa matumizi ya noti hizo kwa mtu mwingine.

No comments:

Post a Comment