Mshambualiaji wa Liverpool Luis Suarez amepewa amri ya
kufanya mazoezi peke yake na kocha Brendan Rodgers,
ambaye amesema hatua hiyo inakuja baada ya mshambuliaji
huyo kuikosea heshima klabu hiyo.
Rodgers pia amekataa taarifa alizotoa Suarez kwamba klabu
ilimhaidi kwamba ikiwa Liverpool watafeli kufuzu kucheza
Champions League.
Suarez, 26, anajipanga kuwasilisha ombi rasmi la kuuzwa wiki
hii ikiwa uhamisho wake utazuiwa.
"Hakujawahi kuwa ahadi yoyote ya namna hiyo baina yetu -
kwa kifupi ahadi yoyote, na kwa maana hiyo hakuna ahadi
iliyovunjwa," alisisitiza Rodgers.
"Klabu na wawakilishi wake walikuwa na mazungumoz kadhaa
na alijua kila kitu kilivyokuwa kinaendelea .
"Ameikosea sana heshima klabu - lakini klabu hii ilimpa na
kumfanyia kila kitu.
"Maneno yake niliyoyasoma kwenye vyombo vya habari
yamenisikitikisha sana - lakini kazi yangu ni kubwa zaidi
ya hili suala. "
Vyanzo vya karibu na Liverpool vinasisitiza uamuzi wa
kumlazmisha Suarez afanye mazoezi kimpango wake
ulifanywa kabla hata mchezaji huyo hajaongea jana na
vyombo vya habari, hivyo uamuzi huo umetokana na
kucheza kwake chini ya kiwango kwenye mechi za kirafiki.
Rodgers aliongeza: "Nitachukua maamuzi magumu juu ya
suala hili. Nadhani Luis anajua sapoti aliyokuwa akipata
kwenye klabu hii na hilo limekuwa jambo la siku zote.
"Kazi yangu ni kupigana na kuilinda klabu hii. Mazungumzo
niliyokuwa nayo na yeye, anajua yalikuwa na yataendelea
kuwa binafsi kati yangu na yeye."
No comments:
Post a Comment